Al Ahly Tripoli mikononi mwa Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 21st August 2024


Al Ahly Tripoli mikononi mwa Simba

Timu ya Al Ahly Tripoli ya Libya huenda ikachuana na Simba katika mechi ya raundi ya kwanza kuwania tiketi ya kucheza hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho barani Afrika msimu huu

Al Ahly Tripoli iliichapa Uhamiaji Fc ya visiwani Zanzibar mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza na timu hizo zitarudiana siku ya Jumamosi kukamilisha raundi ya pili

Mechi zote zinapigwa Libya, Uhamiaji walichagua kucheza nchini humo baada ya CAF kutoupitisha uwanja wa New Amaan Complex

Ni wazi Simba itachuana na Al Ahly Tripoli kuwania tiketi ya makundi CAF CC ambapo mechi zote zitapigwa Septemba 2024 Simba ikitarajiwa kuanzia ugenini na kumalizia nyumbani

Simba haijashiriki hatua ya awali ya michuano hiyo ikiwa miongoni mwa timu zilizokusanya alama nyingi katika rank za CAF

Kulingana na viwango vipya vilivyotolewa na CAF, Simba inashika nafasi ya 7 kwa ubora Afrika


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.