Timu ya Al Ahly Tripoli ya Libya huenda ikachuana na Simba katika mechi ya raundi ya kwanza kuwania tiketi ya kucheza hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho barani Afrika msimu huu
Al Ahly Tripoli iliichapa Uhamiaji Fc ya visiwani Zanzibar mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza na timu hizo zitarudiana siku ya Jumamosi kukamilisha raundi ya pili
Mechi zote zinapigwa Libya, Uhamiaji walichagua kucheza nchini humo baada ya CAF kutoupitisha uwanja wa New Amaan Complex
Ni wazi Simba itachuana na Al Ahly Tripoli kuwania tiketi ya makundi CAF CC ambapo mechi zote zitapigwa Septemba 2024 Simba ikitarajiwa kuanzia ugenini na kumalizia nyumbani
Simba haijashiriki hatua ya awali ya michuano hiyo ikiwa miongoni mwa timu zilizokusanya alama nyingi katika rank za CAF
Kulingana na viwango vipya vilivyotolewa na CAF, Simba inashika nafasi ya 7 kwa ubora Afrika



