Jeuri ya Yanga kwa Mzize iko hapa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th September 2024


Jeuri ya Yanga kwa Mzize iko hapa

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema mshambuliaji Clement Mzize amechagua kuendelea kuwatumikia mabingwa hao wa nchi kutokana na mipango mizuri waliyonayo

Hivi karibuni Yanga ilipokea ofa kutoka kwa klabu za Wydad Athletic, Kaizer Chiefs na nyingine kutoka barani Ulaya kwa ajili ya mshambuliaji huyo kinda

Hata hivyo Yanga iliweka msimamo na kukataa ofa zote wakisisitiza kuwa mchezaji huyo anahitajika katika kufanikisha 'project' ya Yanga

"Kumbakisha Mzize ni moja kati ya mipango tuliyokuwa nayo katika klabu yetu ya Yanga. Mzize ni mchezaji mzuri sana ambaye tunaamini anaweza kuisaidia Yanga ikafikia malengo yake ambayo ni kutwaa ubingwa wa Afrika"

"Ikitokea hii leo Mzize au mfano hata Aziz Ki amesajiliwa na Al Ahly na timu hiyo ikabeba ubingwa wa Afrika, wao binafsi hawawezi kusema kawapa kombe na haitokuwa ajabu sana kwa sababu wameshatwaa kombe hilo mara 11. Lakini mshawahi kujiuliza kama Mzize anabeba kombe la Afrika na Yanga  kwa mara ya kwanza katika historia ni kitu ambacho kitampa heshima kubwa kama mchezaji"

"Lakini pia sisi tunasema hatumuuzi Mzize kwa sababu tunaweza kumtimizia mahitaji yake. Hatuwezi kuwa na jeuri hiyo kama tusingekuwa na fedha," alitamba Kamwe


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.