Simba yajitoa kwa Lawi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th September 2024


Simba yajitoa kwa Lawi

Klabu ya Simba imeachana na mpango wa usajili wa beki Lameck Lawi kutoka klabu ya Coastal Union, imefahamika

Lawi amerejea nchini hivi karibuni baada ya mpango ya kujiunga na KAA Genk ya Ubelgiji kukwama

Mchezaji huyo aliingia kwenye mgogoro baada ya kusaini klabu ya Simba wakati huohuo klabu yake ya Coastal Union ikigoma kumuachia kwa madai Simba haikukamilisha mchakato wa usajili wake kwa wakati

Simba ilipeleka malalamiko yake Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji lakini taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Simba imethibitisha kuwa Wekundu hao wa Msimbazi wamefuta shauri hilo

Simba imechukua uamuzi huo kwa kile kilichoelezwa kuzingatia maslahi ya mchezaji ili kumruhusu aendeleze kukuza kipaji chake

Lawi (18) alipata nafasi ya kwenda kufanya majaribio nchini Ubelgiji hata hivyo hakufanikiwa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.