Transfer - International

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Septemba 14 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Sep 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Septemba 14 2024

Wakala wa mshambuliaji wa Misri Mohamed Salah, 32, ameongeza uvumi kuhusu hatma yake katika klabu ya Liverpool baada ya kutuma kauli ya hasira kwenye mitandao ya kijamii. (Mirror)

Kiungo wa kati wa Ufaransa Adrien Rabiot, 29, ameamua kwamba hatohamia Newcastle United kwa sababu anataka kucheza soka la Ulaya. (Football Insider)

Everton wamedhamiria kusimama na Sean Dyche kwa angalau msimu mzima huku kukiwa na shinikizo kubwa kwa meneja huyo ambaye yuko mkiani mwa Ligi Kuu ya Uingereza. (Telegraph - subscription required)

Mkufunzi wa Newcastle Eddie Howe amedai kuwa baadhi ya wapinzani wao walijaribu kuongeza bei maradufu kwa malengo fulani katika miaka ya mapema baada ya klabu hiyo kunyakua klabu hiyo ikiungwa mkono na Saudi Arabia. (Chronicle Live)

Howe pia alitetea rekodi yake ya uhamisho kama meneja wa Newcastle United katika jibu kali kwa kukosolewa na mkurugenzi mpya wa michezo Paul Mitchell kwamba muundo wa kuajiri wa klabu "haufai kwa madhumuni".(Telegraph - subscription required)

Arsenal na Chelsea zinatarajiwa kumjumuisha mshambuliaji wa Sporting Lisbon na Uswidi Viktor Gyokeres, 26, kwenye orodha yao ya wachezaji watakaowanunua dirisha la usajili la majira ya joto litakapofunguliwa. (Football Insider)

Mkurugenzi wa zamani wa ufundi wa Stoke City,. Ricky Martin yuko kwenye sura ya kuwa mkurugenzi mpya wa michezo wa Carlisle United . (Teamtalk, external)

Chelsea na Tottenham bado wanavutiwa na mlinzi wa Lecce wa Denmark Patrick Dorgu, 19, ambaye thamani yake ni takriban euro 40m (£33.8m). (La Gazzetta dello Sport kupitia SportWitness)

Leeds United walikuwa na ofa ya pauni milioni 8.5 ili kumsaini mchezaji wa kimataifa wa Hungary Roland Sallai lakini winga wa wakati huo wa Freiburg , 27, hakushawishika kuhusu uhamisho wa msimu wa joto na kujiunga na miamba ya Uturuki Galatasaray . (HITC)

Beki wa Chelsea Muingereza Ben Chilwell anatumai kujumuishwa katika kikosi cha wachezaji 25 cha klabu hiyo kinachoshiriki Ligi ya Premia, kwakuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 hatarajiwi kuhamia Uturuki kwa mkopo. (Telegraph - Subscription required)

Mtendaji mkuu wa Liverpool Michael Edwards anaongoza harakati za klabu hiyo za kumtafuta kiungo mpya wa kati. (Football Insider)

BBC

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
1m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
30m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’