Real Madrid watatuma skauti katika mchezo wa Jumapili wa London kaskazini huku wakifikiria kumnunua beki wa Arsenal mwenye umri wa miaka 23 William Saliba na wa kati wa Tottenham na Argentina Cristian Romero, 26. (Defensa Central)
Winga wa Chelsea mwenye umri wa chini ya miaka 20 wa Chelsea Carney Chukwuemeka ni miongoni mwa walengwa wa AC Milan katika dirisha la uhamisho la Januari. (Calciomercato)
Real Madrid wanakaribia kufikia makubaliano ya kumsajili mlinzi wa Bayern Munich Alphonso Davies, 23, kwa uhamisho wa bila malipo, huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Canada akiweza kusaini mkataba wa awali wa kandarasi kuanzia Januari. (AS)
Liverpool wanamtafuta mlinzi wa Sevilla Mfaransa Loic Bade, 24, huku wakifikiria kuchukua nafasi ya mlinzi wa kati wa Uholanzi Virgil van Dijk, 33. (Caught Offside)
Chelsea wanaweza kurejea kumnunua mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen mwenye umri wa miaka 25 mwezi Januari kutokana na kipengeLe cha mapumziko katika mkataba wake wa mkopo huko Galatasaray. (Football Insider)
Barcelona ilikataa ofa ya takribanI pauni milioni 210 kutoka kwa Paris St-Germain kwa winga wa Uhispania Lamine Yamal, 17, mwezi Juni, kulingana na Andy Bara - wakala wa kiungo wa kati wa Barca na hispania Dani Olmo. (Mundo Deportivo)
West Ham wanaendelea kufanyia kazi mpango wa kumsajili beki wa zamani wa Cameroon Joel Matip, 33, kwa uhamisho wa bure. (Football Insider)
Mama na wakala wa Adrien Rabiot anasema kiungo huyo wa kati wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 29, ambaye amekuwa akihusishwa na Newcastle na Manchester United, hatarejea klabu ya zamani ya Juventus. (Mirror)
BBC



