Bao la dakika ya kwanza lililofungwa na Emmanuel Keyeke lilitosha kuihakikishia Singida BS ushindi muhimu wa bao 1-0 dhidi ya Pamba Fc katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa CCM Krumba
Huo ulikuwa ushindi wa nne kwa Singida BS msimu huu vijana wa Kocha Patrick Aussems wakiendeleza rekodi ya ushindi kwa asilimia 100
Singida BS imezidi kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 12
Wakati Singida BS wakiendeleza umwamba, hali bado ni mbaya kwa Coastal Union iliyochapwa mabao 2-0 dhidi ya Namungo Fc katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex
Ulikuwa ushindi wa kwanza kwa Namungo Fc ambayo ilipoteza mechi zote tatu zilizopita huku Coastal Union wakipoteza mechi ya pili



