Singida BS yajichimbia kileleni Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th September 2024


Singida BS yajichimbia kileleni Ligi Kuu

Bao la dakika ya kwanza lililofungwa na Emmanuel Keyeke lilitosha kuihakikishia Singida BS ushindi muhimu wa bao 1-0 dhidi ya Pamba Fc katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa CCM Krumba

Huo ulikuwa ushindi wa nne kwa Singida BS msimu huu vijana wa Kocha Patrick Aussems wakiendeleza rekodi ya ushindi kwa asilimia 100

Singida BS imezidi kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 12

Wakati Singida BS wakiendeleza umwamba, hali bado ni mbaya kwa Coastal Union iliyochapwa mabao 2-0 dhidi ya Namungo Fc katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex

Ulikuwa ushindi wa kwanza kwa Namungo Fc ambayo ilipoteza mechi zote tatu zilizopita huku Coastal Union wakipoteza mechi ya pili


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.