Klabu ya Azam Fc imefungua mazungumzo ya kumuongeza mkataba kiungo wake Feisal Salum 'Fei Toto', hata hivyo nyota huyo amegomea mazungumzo hayo, imefahamika
Fei Toto bado ana mkataba na Azam Fc unaomalizika mwishoni mwa msimu, matajiri hao kutoka Chamazi wanataka kumpa mkataba wa muda mrefu zaidi kwa kuzingatia ubora alionao sasa
Akihojiwa na wanahabari hivi karibuni katika siku ya Azam Media Day, Fei Toto alifichua yuko tayari kwa changamoto mpya katika klabu nyingine
Fei Toto alisema tayari mezani kuna ofa kutoka klabu mbalimbali lakini kwa sasa anaheshimu mkataba wake na Azam Fc
"Mimi ni mchezaji nacheza popote, iwe Simba, Yanga, Azam na hata nje ya nchi kama nitapata nafasi hiyo"
"Kwa sasa nina mkataba na Azam Fc hivyo naheshimu mkataba huo lakini nafahamu kuna timu zimeonyesha nia ya kunihitaji," alisema Fei Toto
Feitoto pia alikanusha uvumi unaodai kuwa hana maelewano mazuri na Rais wa Yanga Injinia Hersi ambapo kiungo huyo alibainisha kuwa amekuwa akiwasiliana na Hersi mara kwa na ni mtu anayemshauri mambo mengi
"Mimi sina tatizo lolote na Injinia Hersi, ni mtu ninaewasiliana nae mara kwa mara na hunishauri vitu vingi. Hakuna tofauti yoyote kati yangu naye"
Kumekuwa na taarifa kuwa Fei Toto yuko tayari kurejea kwa waajili wake hao wa zamani Yanga, baada ya misimu miwili ya kuitumikia Azam Fc
Klabu ya Simba pia inatajwa kumuwania kiungo huyo tegemeo wa timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars'
Katika dirisha la usajili lililopita, Simba walifungua mazungumzo na Azam Fc kwa ajili ya kumsajili Fei Toto lakini Azam Fc hawakuwa tayari kufanya biashara



