Yanga yaalikwa Kenya

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th September 2024


Yanga yaalikwa Kenya

Gavana wa Kaunti ya Siaya nchini Kenya, James Orengo amewasilisha mwaliko rasmi kwa klabu ya Yanga kushiriki ufunguzi wa uwanja wa Siaya Januari 1, 2025

Mwaliko huo uliwasilishwa kwa Rais wa Yanga Injinia Hersi Said ambaye mwishoni mwa wiki alikuwa nchini Kenya kushiriki Kikao cha Kamati ya Utendaji cha Shirikisho la soka barani Afrika (CAF)

Yanga inatarajiwa kuchuana na mabingwa wa Kenya, Gor Mahia katika mchezo wa ufunguzi wa uwanja huo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.