Baada ya mwanzo wa kusuasua katika ligi kuu ya NBC, Azam Fc leo imezinduka na kuifumua KMC mabao 4-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa KMC
Idd Nado, Mwaikenda na Saadun walifunga mabao ya Azam Fc huku Freddy Tangalu akijifunga bao la nne
Ushindi huo ni matokeo muhimu kwa kocha mkuu wa Azam Fc Rachid Taoussi ambaye sasa anaandikisha ushindi wake wa kwanza ukiwa ni mchezo wa pili tangu alipokabidhiwa mikoba iliyoachwa na Yusuph Dabo
Azam Fc imesogea mpaka nafasi ya sita katika msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama tano huku KMC wakiporomoka hadi nafasi ya nane wakiwa na alama nne baada ya mechi nne



