Simba - Local

Fadlu apania ushindi dhidi ya Al Ahli Tripoli

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Sep 2024
Fadlu apania ushindi dhidi ya Al Ahli Tripoli

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amesema maandalizi kuelekea mchezo dhidi ya Al Ahli Tripoli yamekamilika akiwa na matumaini makubwa ya kushinda mchezo huo na hatimaye kufuzu hatua ya makundi CAF CC

Fadlu amesema watakwenda katika mchezo huo wakiwa na mpango mkakati tofauti na ule waliotumia walipokuwa ugenini

"Tulicheza mechi ya kwanza ugenini tukiwa na lengo la kutoruhusu bao na pia kutafuta angalau bao la ugenini"

"Tulifanikiwa mpango wa kwanza wa kutoruhusu bao lakini hatukufanikiwa mpango wa pili wa kufunga bao ugenini"

"Kesho tuko nyumbani lakini tutahitaji kuwa makini ili kuhakikisha haturuhusu wao kufunga bao la ugenini kwani wakifunga bao moja sisi tutalazimika kufunga mawili"

"Hii haimaanishi kwamba tutacheza kama tulivyokuwa ugenini, tutabadilika, tutacheza kwa kushambulia na kuchukua tahadhari katika ulinzi pia"

"Wapinzani wetu bado hawafahamu ni mfumo gani tutatumia katika mchezo huu wa pili hilo ni jambo la faida kwetu, kile walichokishuhudia Libya sio watakachokiona kesho," alisema

Fadlu pia amewataka mashabiki wa Simba kujitokeza kwa wingi uwanja wa Benjamin Mkapa kuwapa hamasa wachezaji wao

"Tunawahitaji mashabiki wa Simba waje kwa wingi uwanjani, naamini wingi wao utatuongezea ari na morali ya kupambana na kufanikisha malengo yetu ya kushinda mchezo"

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
47m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’