Simba iko poti 1 droo ya makundi CAF CC

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd September 2024


Simba iko poti 1 droo ya makundi CAF CC

Baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Al Ahli Tripoli hapo jana na kujihakikishia tiketi ya kucheza hatua ya makundi CAF CC, Mnyama atakuwa katika poti 1 kwenye droo ya makundi itakayofanyika Oktoba 07 Cairo, Misri

Katika poti 1 Simba iko pamoja na vigogo wengine Zamalek, RS Berkane na USM Alger. Habari njema ni kuwa timu hizi hazitakutana katika hatua ya makundi

Kwenye makundi Simba itapangwa dhidi ya timu kutoka poti 2, 3 na zile ambazo hazina alama

Katika poti 2 kuna Asec Mimosas, Stade Malien, Al Masry na CS Sfaxien

Katika poti  3 kuna Enyimba na ASC Jaaraf huku timu nyingine 6 hazina alama zinaunda poti ya 4

Timu hizo ni CS Constantine, Bravos do Maquis, Lunda Sul, Orapa United, Black Bulls na Stellenbosch


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.