Mmiliki mtarajiwa wa Everton Dan Friedkin amemtambua kocha wa timu ya taifa ya England Gareth Southgate, 54, kama mtu anayetarajiwa kuchukua nafasi ya Muingereza mwenzake Sean Dyche, 53, katika uwanja wa Goodison Park. (GiveMeSport)
Liverpool wanajiandaa kuivamia Bayer Leverkusen kwa kiungo wao wa Ujerumani Florian Wirtz, 21, mlinzi wa Uholanzi Jeremie Frimpong, 23, na kiungo wa kati wa Argentina Exequiel Palacios, 25. (CaughtOffside)
The Reds pia wana nia ya kumsajili kiungo wa Uhispania Martin Zubimendi, 25, kutoka Real Sociedad katika msimu wa Januari wa usajili wa wachezaji (Fabrizio Romano, kupitia TeamTalk)
Beki wa Liverpool na England Joe Gomez, 27, anawaniwa na klabu za Aston Villa na Newcastle. (Football Insider)
Real Madrid wanamfuatilia mlinzi wa Nottingham Forest Murillo, 22, lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka Barcelona na Bayern Munich kumpata Mbrazil huyo. (HITC)
Newcastle, Manchester United na Tottenham ni miongoni mwa vilabu vinavyovutiwa na kiungo wa kati wa Lille na Uingereza Angel Gomes, 24. (GiveMeSport)
Barcelona watarajiwa kufanya mazungumzo ya dharura wiki hii kujadili iwapo watamleta mlinda lango asiye na hitaji kuchukua nafasi ya mchezaji wao wa kimataifa wa Ujerumani aliyejeruhiwa Marc-Andre ter Stegen. (ESPN)
Kipa wa zamani wa Barcelona na Manchester City wa Chile Claudio Bravo yuko tayari kustaafu akiwa na umri wa miaka 41 ili kuisaidia klabu hiyo wakati Ter Stegen hayupo. (90min)
Liverpool inatarajiwa kufanya mazungumzo na winga wa Colombia Luis Diaz, 27, kuhusu mpango wa kuongeza mkataba wake hadi 2027 kufuatia mwanzo wake mzuri wa msimu huu. (Football Insider)
Vilabu kadhaa vinamfuatilia winga wa Eintracht Frankfurt aliye na umri wa miaka 20 kutoka Uswidi Hugo Larsson. (Fabrizio Romano)
Southampton wanatumai kumshawishi kiungo wa kati wa Uingereza Tyler Dibling, 18, kusaini kandarasi mpya huku Manchester United wakionyesha nia ya kutaka kumnunua. (GiveMeSport)
Sunderland wanatazamia kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Brighton na Jamhuri ya Ireland Aaron Connolly, 24, kutoka Hull City. (Sun)
Leeds United wana nia ya kuanz8sha mazungumzo ya kandarasi mpya na winga wa Wales Daniel James, 26. (Football Insider)
BBC



