Mghana kuinoa Simba Queens

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th September 2024


Mghana kuinoa Simba Queens

Baada ya kuachana na Kocha Juma Mgunda ambaye mkataba wake umemalizika, Simba Queens leo imemtangaza Yussif Basigi raia wa Ghana kurithi mikoba ya Mgunda

Basigi (52) ametua Simba Queens akitokea Haacas Ladies inayoshiriki ligi kuu ya wanawake Ghana

Basigi amewahi kuinoa timu ya Taifa ya Wanawake ya Ghana na kushinda medali ya dhahabu kwenye All African Games mwaka 2015

Atakuwa na kasi ya kuisuka upya Simba Queens ambayo mwezi uliopita ilikosa ubingwa wa CECAFA na hivyo kupoteza nafasi ya kushiriki ligi ya mabingwa ya Wanawake

Jukumu lake la kwanza ni kuhakikisha Simba Queens inatwaa Ngao ya Jamii, mechi ya nusu fainali ikicheza na watani zao Yanga Princess Oktoba 02


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.