Baada ya kuachana na Kocha Juma Mgunda ambaye mkataba wake umemalizika, Simba Queens leo imemtangaza Yussif Basigi raia wa Ghana kurithi mikoba ya Mgunda
Basigi (52) ametua Simba Queens akitokea Haacas Ladies inayoshiriki ligi kuu ya wanawake Ghana
Basigi amewahi kuinoa timu ya Taifa ya Wanawake ya Ghana na kushinda medali ya dhahabu kwenye All African Games mwaka 2015
Atakuwa na kasi ya kuisuka upya Simba Queens ambayo mwezi uliopita ilikosa ubingwa wa CECAFA na hivyo kupoteza nafasi ya kushiriki ligi ya mabingwa ya Wanawake
Jukumu lake la kwanza ni kuhakikisha Simba Queens inatwaa Ngao ya Jamii, mechi ya nusu fainali ikicheza na watani zao Yanga Princess Oktoba 02



