Kamwe awashukia wanaoponda ushindi wa Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd October 2024


Kamwe awashukia wanaoponda ushindi wa Yanga

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema malengo ya timu katika kila mechi ni kukusanya alama tatu

Kamwe amewataka mashabiki na wanachama na timu hiyo kutoingia mtegoni na kuamini ushindi wa bao 1-0 sio matokeo ambayo timu yao inastahili

Baada ya ushindi wa bao 1-0 katika mechi mbili zilizopita dhidi ya Ken Gold na KMC, leo Yanga itashuka tena uwanja wa Azam Complex kumenyana na Pamba Jiji. Kamwe amesema lengo kuu katika mchezo huo ni kupata alama tatu

"Wachezaji wote wa Yanga wanafurahia ushindi wa alama tatu, sababu ukipata goli moja si kwamba unapata pointi moja, ukipata goli moja na anayefunga goli mia mnapata wote pointi tatu"

"Haya maneno yanayotengenezwa makusudi kutia presha kwa wachezaji wetu, niwaambie kitu, Yanga tunawachezaji wakomavu kweli kweli na wanauwezo wakumudu hizo presha na kucheza kwenye kiwango kizuri kabsa"

"Nafikiri kwa mtu anayeelewa mpira ni kwamba kuwa tishio kwenye mpira ni kushinda mechi, unapokuwa tishio na haushindi mechi ni mbaya zaidi, ukifanya tathmini kuanzia kwenye pre season tumefungwa mchezo mmoja tu na Ausburg kwenye kila mechi tumeweza kufunga goli na sisi tunaweza kushinda kila mechi," alisema Kamwe


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.