Transfer - International

Tetesi za usajili Ulaya, Ijumaa Oktoba 4 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Oct 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Ijumaa Oktoba 4 2024

Paris St-Germain wanaongoza katika kinyang'anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa Misri Mohamed Salah na watajaribu kumjaribu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32, ambaye mkataba wake wa Liverpool unamalizika mwishoni mwa msimu huu, kwa mkataba wa miaka mitatu. (sun)

Liverpool wamemtambua fowadi wa Borussia Dortmund Karim Adeyemi kama mrithi wa Salah, na wako tayari kutoa dau la pauni milioni 41 kumnunua Mjerumani huyo mwenye umri wa miaka 22. (Bild - Deutsch)

Manchester United inaandaa ofa ya takriban pauni milioni 34 kumnunua winga wa Benfica mwenye umri wa miaka 25 na Uturuki Kerem Akturkoglu. (Fichajes – In Spanish)

Newcastle United wanataka kurejelea harakati zao za kutaka kumnunua beki wa kati wa England Marc Guehi mwezi Januari, huku wakitarajiwa kuwa Crystal Palace watakuwa tayari kumuuza mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (Mail – ubscription Required )

Chelsea inamtaka fowadi wa Colombia Jhon Duran, lakini Aston Villa wanataka zaidi ya £80m kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20. (TeamTalks)

Barcelona na Juventus wanafuatilia hali ya winga wa Argentina Alejandro Garnacho, 20, huku Manchester United ikiaminika kumthamini mchezaji huyo kwa pauni milioni 50. (Sun)

Mkufunzi wa Fenerbahce Jose Mourinho anagombea kuchukua nafasi ya Sean Dyche kama meneja wa Everton mara tu Dan Friedkin atakapomaliza kuinoa klabu hiyo. (Football Insider),. Atletico Madrid wamemtambua mlinzi wa Chelsea na England Ben Chilwell, 27, kama lengo lao la hivi punde la uhamisho. (TeamTalks)

Newcastle United ni miongoni mwa walio mstari wa mbele kumsajili mshambuliaji wa Canada Jonathan David mwenye umri wa miaka 24 kutoka Lille. (GiveMeSport)

Mshambulizi wa Norway Erling Haaland, 24, anatazamiwa kusaini mkataba mpya na Manchester City lakini anataka kipengele cha kuachiliwa kwa pauni milioni 100 kiongezwe. (TeamTalks) Barcelona wanafanya usajili wa Haaland katika dirisha la uhamisho la 2025 kuwa kipaumbele chao. (SPORT - Spanish)

Sir Jim Ratcliffe atahudhuria mechi ya Ligi Kuu ya Manchester United huko Aston Villa Jumapili huku uvumi kuhusu mustakabali wa meneja Erik ten Hag ukiongezeka. (Mirror)

BBC

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
1m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
29m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’