Msimu mpya wa Ligi Kuu ya wanawake Tanzania Bara 2024/2025 linafunguliwa leo kwa michezo mitano viwanja tofauti
Bingwa wa simu uliopita Simba Queens itaanza kampeni kutetea taji hilo dhidi ya Mlandizi Queens kwenye uwanja wa Kituo cha Ufundi cha TFF, Kigamboni Dar es salaam
Miamba mingine ya soka la wanawake Yanga Princess itaanza kampeni ugenini dhidi ya Bunda Queens kwenye uwanja wa Karume mjini Musoma mkoa wa Mara.
Bingwa wa Ngao ya Jamii kwa wanawake, JKT Queens itakuwa mgeni wa Alliance Girls kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kuwania pointi za mchezo wa kwanz
Ilyokuwa Amani Queens ambayo sasa inaitwa Mashujaa Queens itaikaribisha Gets Program iliyopanda daraja kwenye uwanja wa Maj Gen Isamuhyo ulipo Mbweni, Dar es Salaam
Fountain Gate Princess wao watawakaribisha Ceasiaa Queens kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.



