Ligi Kuu ya Wanawake kuanza leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 9th October 2024


Ligi Kuu ya Wanawake kuanza leo

Msimu mpya wa Ligi Kuu ya wanawake Tanzania Bara 2024/2025 linafunguliwa leo kwa michezo mitano viwanja tofauti

Bingwa wa simu uliopita Simba Queens itaanza kampeni kutetea taji hilo dhidi ya Mlandizi Queens kwenye uwanja wa Kituo cha Ufundi cha TFF, Kigamboni Dar es salaam

Miamba mingine ya soka la wanawake Yanga Princess itaanza kampeni ugenini dhidi ya Bunda Queens kwenye uwanja wa Karume mjini Musoma mkoa wa Mara. 

Bingwa wa Ngao ya Jamii kwa wanawake, JKT Queens itakuwa mgeni wa Alliance Girls kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kuwania pointi za mchezo wa kwanz

Ilyokuwa Amani Queens ambayo sasa inaitwa Mashujaa Queens itaikaribisha Gets Program iliyopanda daraja kwenye uwanja wa Maj Gen Isamuhyo ulipo Mbweni, Dar es Salaam

Fountain Gate Princess wao watawakaribisha Ceasiaa Queens kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.