Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amesema haitakuwa kazi rahisi kwa Simba kutinga robo fainali ya kombe la Shirikisho lakini wamejipanga na watahakikisha wanafanikisha malengo hayo
Droo ya makundi ya CAF CC ilifanyika Misri juzi Simba ikipangwa kundi A na timu za CS Sfaxien, CS Constantine na Bravos
"Ni kundi gumu, Bravos ni timu nzuri, CS Sfaxien na CS Constantine zinatoka Afrika Kaskazini ni timu nzuri pia"
"Tuna faida kidogo kwa sababu tulicheza na Al Ahly Tripoli katika hatua iliyopita, hivyo wachezaji wangu wamepata uzoefu juu ya nini tunapaswa kufanya tutakapokwenda Algeria na Tunisia"
"Haitakuwa rahisi kwa sababu wachezaji wetu wengi hawana uzoefu na michuano hii ya CAF, lakini tutakwenda kushindana"
"Lengo letu kuu ni kuhakikisha tunamaliza nafasi ya kwanza katika kundi. Kuna faida ya kumaliza juu katika kundi kwani kwenye robo fainali utacheza dhidi ya timu iliyomaliza katika nafasi ya pili kwenye kundi jingine ingawa haimaanishi itakuwa mechi rahisi," alisema Fadlu
Simba itaanzia nyumbani katika hatua ya makundi ambapo mechi ya kwanza dhidi ya Bravos itapigwa Novemba 27 katika uwanja wa Benjamin Mkapa



