Stars katika mtego wa DR Congo Jumanne

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th October 2024


Stars katika mtego wa DR Congo Jumanne

Jumanne, Oktoba 15 2024 timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' itakuwa uwanja wa Benjamin Mkapa katika mchezo wa marudiano kuwania kufuzu Afcon 2025 dhidi ya DR Congo

Baada ya kupoteza mchezo wa kwanza baina ya timu hizo uliopigwa dR Congo juzi, Jumanne Tanzania inahitaji ushindi tu ili kuweka hai matumaini ya kufuzu Afcon 2025

Katika msimamo wa kundi H, DR Congo wako kileleni wakiwa alama 9, wako katika nafasi nzuri ya kufuzu na pengine watakuja wakiwa lengo la kusaka ushindi ili kujihakikishia tiketi yao mapema

Tanzania iko nafasi ya pili ikiwa na alama nne, kama itashinda dhidi ya DR Congo itafikisha alama 7 na kuendelea kusalia nafasi ya pili 

TFF ilitangaza viingilio vya mchezo huo jana ambapo Mzunguuko ni Tsh 2,000/- tu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.