Yanga - Simba - Azam - Singida - Local

TPLB katika mtihani wa ratiba Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
17 Oct 2024
TPLB katika mtihani wa ratiba Ligi Kuu

Uwepo wa Fainali za Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wanaocheza Ligi za Ndani (CHAN), kumetajwa kuwa kutaathiri moja kwa moja ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Almasi Kasongo, alisema mabadiliko ya ratiba za Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kwenye michuano ya CHAN na Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho, moja kwa moja yataathiri ratiba hiyo, hivyo watakaa na kufanya marekebisho

"Tunaendela kufanya marekebisho na maboresho ya ratiba baada ya Kamati ya Utendaji ya CHAN kukaa na kufanya marekebisho ya ratiba zao. Fainali ya CHAN zimepangwa kufanyika hapa Tanzania, Kenya na Uganda kuanzia Februari Mosi mpaka 28, lakini pia kuna mechi za 'play off' za kwenda kucheza hizo fainali ambazo zitaanza Oktoba 25 hadi 27, maana yake wamekuja kuathiri ratiba yetu moja kwa moja," alisema Kasongo

Alisema pia kutokana na hayo, ni lazima wafanye marekebisho ya ratiba ya Ligi Kuu ili kuruhusu wachezaji watumikie timu yao ya taifa. Mbali na hilo, Kasongo pia alisema CAF imebadilisha pia ratiba za Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho ambalo kwa kawaida lilitakiwa lichezwe mwezi Oktoba, sasa linararajiwa kuanza Novemba hadi Januari hivyo kuathiri pia Kombe la Mapinduzi ambalo hufanyika Januari Mosi hadi 13 mwakani

"Januari kuna Kombe la Mapinduzi, lakini kwenye ratiba ya CAF kutakuwa na michezo ya Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho timu za Simba na Yanga zikiwapo. Ikumbukwe Simba na Yanga kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi, lakini kipindi hicho watakuwa kwenye mechi za makundi, ingawa kwa hili sitaki sana kuelezea, kamati yenyewe ipo na klabu zipo zinaweza kulisemea, ila kwetu sisi tutalazimika kufanya marekebisho ya ratiba kutokana na kalenda hiyo ya CAF, kupisha CHAN na mechi za kimataifa," alisema Kasongo

IPP Media

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
38m ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
51m ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
1h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
4h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
8h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
9h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
10h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
11h ago
READ MORE β†’