Transfer - International

Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi Oktoba 17 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
17 Oct 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi Oktoba 17 2024

Real Madrid wameufanya usajili wa mlinzi wa Liverpool na Uingereza Trent Alexander-Arnold, 26, kuwa kipaumbele. (Athletic – Subscription needed) Liverpool na Manchester City wanavutiwa na Nicolo Barella wa Inter Milan, 27, lakini kiungo huyo wa kati wa Italia yuko kwenye rada za Real Madrid na Atletico Madrid. (Fichajes – In Spanish)

Arsenal wanafuatilia maendeleo ya mshambuliaji wa Red Bull Salzburg na Slovenia Benjamin Sesko, 21, huku wakianza kujipanga kwa ajili ya usajili wa dirisha lijalo. (Football London)

Crystal Palace haiko tayari kukaribisha ofa zozote kwa mshambuliaji wa Senegal Ismaila Sarr, 26, mwezi Januari. (Football Insider)

Manchester United wamemuongeza mkufunzi wa Uturuki na mshambuliaji wa zamani wa Italia Vincenzo Montella, 50, kwenye orodha yao ya watu wanaotarajiwa kuchukua nafasi ya mkufunzi wa Uholanzi Erik ten Hag, 54, Old Trafford. (Ajansspor – in Turkish)

Ten Hag atalazimika kuboresha matokeo na kiwango cha mchezo Manchester United ikiwa anataka kusalia katika timu hiyo baada ya mapumziko yajayo ya kimataifa. (Mirror), nje

Manchester United wanapanga wachezaji wa kiungo cha kati watakaochukua nafasi ya kiungo wa kimataifa wa Denmark Christian Eriksen, 32, pamoja na mchezaji wa kimataifa wa Brazil Casemiro, 32. (Football Insider)

United pia wako tayari kumsajili kiungo wa kati wa Uholanzi Frenkie de Jong, 27, ikiwa ataondoka Barcelona msimu ujao. (Fichajes – In Spanish)

Real Madrid wanafikiria kumnunua mchezaji wa kimataifa wa Uingereza Josh Acheampong Januari 18, huku Liverpool, Newcastle na Tottenham pia wakimtaka beki huyo wa kulia wa Chelsea. (Independence)

Crystal Palace wanamtafuta David Moyes, 61, kuchukua nafasi ya meneja Oliver Glasner, 50, baada ya kuanza vibaya msimu wa Ligi Kuu ya Uingereza. (Caughtoffside)

Uteuzi wa Thomas Tuchel kama meneja wa Uingereza umeongeza matumaini ya Newcastle ya kumsajili mlinzi wa Uingereza na Crystal Palace Marc Guehi, 24, huku Eddie Howe sasa akiwa na uwezekano mkubwa wa kusalia St James' Park. (Givemesport)

Liverpool wako kwenye mazungumzo na Sevilla kuhusu kumnunua mlinzi wa Ufaransa Loic Bade, 24. (Todo Fichajes – In Spanish)

Kiungo wa kati wa Newcastle United Isaac Hayden, 29, amekubali kuiwakilisha Jamaica katika ngazi ya kimataifa, baada ya hapo awali kuichezea Uingereza katika kila kundi la umri kutoka chini ya miaka 16 hadi chini ya miaka 21. (TeamTalks)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’