Baada ya kuiongoza Mtibwa Sugar kushinda mechi nne mfululizo ligi ya Championship, Kocha Mellis Nedo anaelekea kujiunga na Kagera Sugar
Wiki iliyopita Kagera Sugar iliachana na Kocha Paul Nkata baada ya mfululizo wa matokeo mabaya
Medo tayari ameaga Mtibwa Sugar ambapo nafasi yake imekaimiwa Awadh Juma aliyekuwa Kocha Msaidizi
Medo ni kocha mwenye uzoefu mkubwa na ligi kuu akiwa amewahi kuzinoa klabu za Coastal Union na Dodoma Jiji kabla ya kurejea kwao



