Uingereza imemtangaza kocha Thomas Tuchel kuwa kocha mpya wa timu ya taifa hilo. Chama cha Soka nchini humo FA kimempa Mjerumani huyo jukumu la kujaribu kutwaa taji lao la kwanza tangu mwaka 1966
Tuchel ambaye amewahi kuwa meneja wa klabu ya Chelsea ataanza kibarua chake Januari mosi mwakani
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 51, ambaye amekuwa kando tangu aagane na Bayern Munich mwishoni mwa msimu uliopita, anarithi mikoba ya Muingereza Gareth Southgate kama kocha wa kudumu
Anakuwa meneja wa tatu wa kigeni wa England baada ya Sven-Goran Eriksson na Fabio Capello
Tuchel, ambaye pia amezifundisha Borussia Dortmund na Paris Saint-Germain, anapewa matumaini ya kumaliza ukame wa miaka 58 wa England kushinda mashindano makubwa tangu Kombe la Dunia la 1966 kwenye ardhi ya nyumbani