Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amemwagia sifa kiungo mahiri wa timu hiyo Debora Fernandez kwa mwendelezo mzuri wa kiwango chake
Tangu aliposajiliwa na Simba, Fernandez amekuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha kocha Fadlu Davids
Kuelekea mchezo wa Kariakoo Derby utakaopigwa Jumamosi katika uwanja wa Benjamin Mkapa, Fernandez anatizamwa kama moja ya wachezaji watakaoibeba Simba mabegani katika mchezo huo
Ahmed amesema kiungo huyo bado hajaonyesha uwezo wake kwa asilimia 100, anachokionyesha sasa ni kama asilimia 15 tu
"Tanzania hii hakuna mchezaji anayefikia walau theluthi ya kiwango cha Debora Mavambo Fernandez na hapo ana asilimia 15 za ubora wake"
"Hapo bado anaendelea kujitafuta na kuendelea kuzoea mazingira na kocha Fadlu anaendelea kumuongezea mambo ya kiufundi"
"Baada ya muda mfupi Fernandez atafanya mambo makubwa sana kwenye mpira wetu," alisema Ahmed



