Yanga yaendeleza ubabe dhidi ya Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th October 2024


Yanga yaendeleza ubabe dhidi ya Simba

Bao la kujifunga Kelvin Kijiri limeihakikishia Yanga ushindi muhimu wa bao 1-0 dhidi ya mahasimu wao Simba katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Mpira wa adhabu uliopigwa Clatous Chama dakika ya 86 uliokolewa na mlinda lango wa Simba Moussa Camara na kutua mguuni kwa Maxi Nzengeli ambaye shuti lake lilimgonga Kijiri na kujaa kimiani

Ilikuwa mechi nzuri yenye ushindani kutoka kwa kila upande, pengine ulikuwa mchezo ambao matokeo ya sare yasingewashangaza wengi

Simba ilipata nafasi adimu mapema katika kipindi cha kwanza lakini Lionel Ateba alishindwa kutumia vyema pasi mpenyezo aliyopewa na Joshua Mutale

Baada ya ushindi huo, Yanga imepanda hadi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 15


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.