Bao la kujifunga Kelvin Kijiri limeihakikishia Yanga ushindi muhimu wa bao 1-0 dhidi ya mahasimu wao Simba katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Mpira wa adhabu uliopigwa Clatous Chama dakika ya 86 uliokolewa na mlinda lango wa Simba Moussa Camara na kutua mguuni kwa Maxi Nzengeli ambaye shuti lake lilimgonga Kijiri na kujaa kimiani
Ilikuwa mechi nzuri yenye ushindani kutoka kwa kila upande, pengine ulikuwa mchezo ambao matokeo ya sare yasingewashangaza wengi
Simba ilipata nafasi adimu mapema katika kipindi cha kwanza lakini Lionel Ateba alishindwa kutumia vyema pasi mpenyezo aliyopewa na Joshua Mutale
Baada ya ushindi huo, Yanga imepanda hadi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 15



