Simba yaunguruma Mbeya, yaichapa Prisons

Joel JJ By Joel JJ β€’ 22nd October 2024


Simba yaunguruma Mbeya, yaichapa Prisons

Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc wamepata alama tatu muhimu mkoani Mbeya baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo uliopigwa uwanja wa Sokoine

Che Fondoh Malone alifunga bao pekee la Simba mapema dakika ya 5 kipindi cha kwanza akimalizia mpira uliotemwa na mlinda lango wa Prisons Mussa Mbissa baada ya mpira wa adhabu uliopigwa na Kibu Denis

Simba ilitawala mchezo huo na pengine wekundu wa Msimbazi walistahili kupata ushindi mnono lakini ufanisi mbele ya lango ilikuwa changamoto

Ni alama tatu muhimu kwa Simba ambazo zimewarudisha katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi huku Prisons wakichechemea baada ya kupoteza mechi ya pili mfululizo katika uwanja wao wa nyumbani


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.