Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc wamepata alama tatu muhimu mkoani Mbeya baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo uliopigwa uwanja wa Sokoine
Che Fondoh Malone alifunga bao pekee la Simba mapema dakika ya 5 kipindi cha kwanza akimalizia mpira uliotemwa na mlinda lango wa Prisons Mussa Mbissa baada ya mpira wa adhabu uliopigwa na Kibu Denis
Simba ilitawala mchezo huo na pengine wekundu wa Msimbazi walistahili kupata ushindi mnono lakini ufanisi mbele ya lango ilikuwa changamoto
Ni alama tatu muhimu kwa Simba ambazo zimewarudisha katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi huku Prisons wakichechemea baada ya kupoteza mechi ya pili mfululizo katika uwanja wao wa nyumbani



