Yanga imeendelea kugawa dozi katika ligi kuu ya NBC leo ikiichapa JKT Tanzania mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex
Mabao ya kipundi cha kwanza yaliyofungwa na Pacome Zouzoua na Clatous Chama yalitosha kuihakikishia Yanga alama tatu muhimu ambazo zimewarudisha katika nafasi ya pili
Ni ushindi wa 6 mfululizo kwa Yanga kwenye ligi huku Wananchi wakiwa wamefunga mabao 11 pasipo kuruhu nyavu zao kutikiswa
Yanga ndio timu pekee ambayo haijaruhusu bao, mlinda lango Djigui Diarra akiwa na cleensheet 6



