Rais wa CAF Patrice Motsepe anasema ipo haja ya kukabiliana na ukosefu wa uanamichezo miongoni mwa nchi za Afrika, ambao umekuwepo kwa muda mrefu
Soka la Afrika limekuwa likikabiliwa na uhasama kati ya nchi au vilabu kwa muda mrefu. Baadhi ya mifano inaweza kuwa timu za uenyeji kushindwa kutoa usafiri wa kutosha, malazi, au vifaa vya mafunzo
Tukio la hivi karibuni la aibu ni pale ambapo mechi ya kufuzu AFCON 2025 kati ya Nigeria na Libya ilibidi kusitishwa. Hii ni baada ya Super Eagles kutumia saa 20 kukwama kwenye Uwanja wa Ndege wa Libya
"Nimesikia hadithi nyingi sana za klabu ya soka au timu ya taifa kwenda nchi fulani. Unatumia saa nyingi kwenye uwanja wa ndege, na wanakuuliza kuhusu hati"
"Inavyoonekana, wakati wa COVID-19, wangeangalia ni wachezaji gani bora kutoka kwa timu yako na kusema wachezaji hao 10 wana COVID-19,"Motsepe alisema wakati wa Mkutano Mkuu wa Kawaida wa 46 wa CAF mjini Addis Ababa, Ethiopia
"Unawaambia kuwa umepimwa, na wanasema hapana, una COVID. Lakini ni ukosefu huu wa uanamichezo ambao umekuwepo, na hatujachukua hatua madhubuti. Iwapo kutakuwa na ukiukwaji wa kanuni na sheria hizo, tutachukua hatua"



