Mgunda kuanza na Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th October 2024


Mgunda kuanza na Simba

Jana klabu ya Namungo Fc ilimtangaza Juma Mgunda kuwa kocha wake mkuu akichukua nafasi ya Mwinyi Zahera aliyebadilishiwa majukumu katika timu hiyo kutoka Ruangwa mkoani Lindi

Kibarua cha kwanza cha Mgunda ni mchezo dhidi ya Simba ambao utapigwa uwanja wa KMC Complex kesho Ijumaa

Unaweza kusema baada ya kufanya kazi nzuri iliyomfanya apendwe na mashabiki wengi wa Simba, Mgunda sasa anakwenda kukabiliana na waajiri wake hao wa zamani

Mgunda alikuwa sehemu ya taasisi ya Simba kwa takribani misimu mitatu akiwa Kocha Mkuu, Kocha wa muda na kazi yake ya mwisho alikuwa Kocha wa Simba Queens

Simba ilitangaza kuachana nae mwezi uliopita baada ya mkataba wake kumalizika

Hata hivyo kazi yake haitakuwa rahisi hapo kesho kwani Mnyama anazihitaji alama zote tatu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.