Klabu za Simba na Yanga zimetajwa kuwania tuzo za klabu bora ya mwaka katika tuzo za mwaka za CAF ambazo zitafanyika Morocco mwishoni mwa mwaka huu
Tuzo hizo zitaandaliwa katika jiji la kitalii la Marrakech, Morocco, tarehe 16 Desemba 2024, Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limetangaza
Hii ni mara ya tatu mfululizo Morocco kuandaa sherehe hizo, baada ya kuandaa kwa mafanikio makubwa katika miaka miwili iliyopita
Yanga na Simba zimeingia pamoja katika tuzo hizo baada ya kufanya vizuri katika michuano ya ligi ya mabingwa msimu uliopita ambapo zote zilicheza hatua ya robo fainali
Hata hivyo mabingwa wa Afrika Al Ahly wamo kama ilivyo kwa mabingwa kombe la Shirikisho ambao pia ni mabingwa wa CAF Super Cup, Zamalek
Vigogo hawa ndio wanapewa nafasi ya kushinda tuzo hiyo iliyokwenda kwa Al Ahly msimu uliopita
Golikipa wa Yanga na timu ya Taifa ya Mali Djigui Diarra ametajwa katika kinyan'ganyiro cha kuwania tuzo ya golikipa bora wa mwaka akichuana na magolikipa wengine bora walioteuliwa kuwania tuzo hiyo akiwemo Andre Onana golikipa wa Manchester United



