Tottenham Hotspur imeendeleza matokeo mazuri katika Ligi ya Europa kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya AZ Alkmaar Alhamisi kwenye Uwanja wa Tottenham Hotspur
Kocha Ange Postecoglou alifanya mabadiliko manane kutoka kwa ushindi wa wikendi dhidi ya West Ham, Spurs ilionekana kuzembea katika kipindi cha kwanza ikionekana kutokuwa na mfumo bora zaidi ya uchezaji
Pengine hilo ilitokana na mabadiliko ya wachezaji wengi ambao hawatumiki mara kwa mara katika kikosi cha kwanza
Richarlison alifunga bao pekee kwa mkwaju wa penalti na kusaidia Tottenham kudumisha mwanzo wao mzuri katika Ligi ya Europa
Ulikuwa mchezo wa kwanza kwa Richarlison kuichezea Spurs msimu huu baada ya kupata majeraha, Mbrazil huyo alibishana kwa muda mfupi na James Maddison kuhusu nani apige penalti baada ya Maxim Dekker kumuangausha Lucas Bergvall kwenye eneo la hatari
Nahodha Maddison aliacha jukumu hilo na Richarlison alituma mpira chini moja kwa moja katikati na kuipatia Tottenham bao la muhimu dakika ya 53



