Derby ya pacha iliyopigwa uwanja wa CCM Liti, mkoani Singida mchana wa leo imemalizika kwa wenyeji Singida Black Stars kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Fountain Gate
Mchezo huo ulianza kwa kasi timu zikishambuliana kwa zamu lakini ni Singida Black Stars waliotumia vyema nafasi kwa kufunga mabao yao katika kipindi cha pili kupitia kwa Josphat Bada na Ayoub Lyanga
Ushindi muhimu na wenye maana kubwa kwa Singida BS ambayo imezidi kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 22
Mchezo wao unaofuata ni dhiidi ya mabingwa watetezi wa ligi hiyo Yanga ukitarajiwa kupigwa uwanja wa New Amaan Complex, Jumatano Oktoba 30

