Manchester United wanafanya mazungumzo na wagombea wa ukocha kuchukua nafasi ya Erik ten Hag, Kevin de Bruyne anaweza kuondoka Manchester City na kujiunga na klabu ya MLC na Eintracht Frankfurt yatangaza thamani ya Omar Marmoush anayenyatiwa na Liverpool
Manchester United tayari wamefanya mazungumzo na makocha kadhaa miongoni mwao Xavi Hernandez na Ruben Amorim wa Sporting Lisbo huku shinikizo la kumtimua Mholanzi Erik ten Hag, likizidi kuongezeka. (Daily Mail)
Kiungo wa kati wa Manchester City Kevin de Bruyne, 33, anaweza kuhamia San Diego FC inayoshiriki Ligi Kuu ya Soka ya Marekani, mkataba wa Mbelgiji huyo ukikamilika mwezi Juni mwakani. (GiveMeSport)
Eintracht Frankfurt wameweka thamani ya kati ya euro milioni 50-60 kwa mshambuliaji wa Misri Omar Marmoush, 25, ambaye wawakilishi wake wamefanya mazungumzo na Liverpool. (Sky Germany)
BBC



