Mechi mbili Ligi Kuu zinapigwa leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th October 2024


Mechi mbili Ligi Kuu zinapigwa leo

Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ikiingia mzunguuko wa 10 mechi mbili zikitarajiwa kupigwa katika viwanja tofauti

Baada ya kuchezea kichapo katika derby ya pacha, Fountain Gate watakuwa nyumbani Manyara kuumana na Mashujaa Fc mchezo ukitarajiwa kupigwa saa 10 jioni

Namungo Fc ambao pia walipoteza mchezo uliopita dhidi ya Simba, wamerejea nyumbani uwanja wa Majaliwa kuikaribisha Pamba Jiji mchezo utakaopigwa saa 1 usiku


  


XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.