Ligi Kuu Tanzania Bara inaendelea leo kwa michezo miwili kufanyika Arusha na Mbeya
Coastal Union itakuwa mwenye wa Kagera Sugar kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha
Coastal ipo nafasi ya 12 katika msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 8 baada ya michezo tisa wakati Kagera Sugar ni ya 14 ikiwa pointi 5 baada ya michezo nane
Mechi nyingine, Dodoma Jiji itakuwa mgeni wa Ken Gold katika uwanja Sokoine jijini Mbeya
Dodoma Jiji inashika nafasi ya saba ikiwa pointi 12 baada ya michezo tisa wakati Ken Gold ni ya 16 mwisho wa msimamo ikiwa na pointi 4
Mchezo kati ya Simba na JKT Tanzania uliokuwa ufanyika leo umeahirishwa kutokana na baadhi ya wachezaji wa JKT kuwa na majeraha baada ya basi walilokuwa wakisafiria kupinduka wakati wakitoka Dodoma kwenye mchezo dhidi ya Dodoma Jiji



