Mashujaa Fc kutoka mkoani Kigoma imetamba itaendeleza ubabe dhidi ya Wekundu wa Msimbazi Simba Sc pale timu hizo zitakapokutana katika mchezo wa ligi kuu siku ya Ijumaa, Novemba 1
Nyasi za uwanja wa Lake Tanganyika zitakuwa kwenye wakati mgumu katika mchezo huo utakaopigwa saa 10 jioni
Mashujaa Fc wanakumbukumbu ya kuibuka na ushindi dhidi ya Simba mara ya mwisho katika uwanja huo msimu uliopita kwenye mchezo wa hatua ya mtoano kombe la Shirikisho la CRDB Mashujaa wakitinga robo fainali kwa ushindi wa mikwaju ya penati 4-3
Hata hivyo Mashujaa Fc hawajawahi kuifunga Simba katika mechi za ligi kuu, ubabe wao wameufanya katika michuano ya kombe la FA
Je wataweza kuwazuia vijana wa Kocha Fadlu Davids ambao wameshinda mechi zote walizocheza ugenini msimu huu?




