Local,Normal News,Yanga, Singida

Aussems afurahia kucheza New Amaan Complex

Joel JJ By Joel JJ
β€’
29 Oct 2024
Aussems afurahia kucheza New Amaan Complex

Kocha Mkuu wa Singida Black Stars Patrick Aussems amesema ubora wa uwanja wa New Amaan Complex utawapa faida kimbiinu katika mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya Yanga ambao utapigwa Jumatano usiku

Akizungumza katika Mkutano na wanahabari kuelekea mchezo huo, Aussems alisema kikosi chake kina wachezaji wengi bora hivyo kesho itakuwa nafasi nzuri kwao kuonyesha walichonacho

"Tunatumia uwanja wa LITI kule Singida ambao hauna ubora kama uwanja huu wa Amaan. Naamini kucheza hapa ni faida kwetu kwani tuna wachezaji wengi wazuri ambao wako tayari kucheza dhidi ya Yanga"

"Itakuwa mechi ya wazi ambayo inazikutanisha timu zilizofanya vizuri mpaka sasa. Sote hatujapoteza mchezo wenzetu hawajaruhusu bao, nikuhakikishie itakuwa mechi yenye ushindani mkubwa," alisema Aussems

Nae Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo huo licha ya changamoto ya ratiba ya kucheza mechi mfululizo

"Kwanza nina furaha kurejea tena hapa Zanzibar, kila Yanga inapokwenda huwa inategemea Ushindi, tupo hapa kwaajili ya Kushinda ingawa tunatambua Singida wana Kikosi kizuri na wamepata muda mrefu wa Kujiandaa," alisema Gamondi

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
4h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
5h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
12h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
13h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
14h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
15h ago
READ MORE β†’