Mchezo wa ligi kuu ya NBC baina ya Young Africans dhidi ya Azam utachezwa katika uwanja wa Azam complex-Chamazi badala ya Benjamini Mkapa
Bodi ya ligi imetaja sababu ya mabadiliko haya ni marekebisho makubwa yanayoendelea kufanyika katika uwanja wa Mkapa. Mchezo huu utachezwa Novemba 2,2024
Uwanja wa Benjamini Mkapa unaendelea kuboreshwa tayari kwa ajili ya michuano ya CHAN 2025 ambayo yatafanyika kuanzia Februari 2025 katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda
Aidha maboresho hayo ni sehemu ya maandalizi pia ya AFCON 2027 ambayo itachezwa katika ardhi ya Tanzania,Kenya na Uganda
Katika hatua nyingine, Bodi ya ligi pia imeidhinisha mchezo wa ligi kuu kati ya Singida Black Stars dhidi ya Coastal Union kupigwa katika uwanja wa New Amaan Complex, Novemba 02



