Yanga vs Azam Fc kupigwa Azam Complex

Joel JJ By Joel JJ β€’ 30th October 2024


Yanga vs Azam Fc kupigwa Azam Complex

Mchezo wa ligi kuu ya NBC baina ya Young Africans dhidi ya Azam utachezwa katika uwanja wa Azam complex-Chamazi badala ya Benjamini Mkapa

Bodi ya ligi imetaja sababu ya mabadiliko haya ni marekebisho makubwa yanayoendelea kufanyika katika uwanja wa Mkapa. Mchezo huu utachezwa Novemba 2,2024

Uwanja wa Benjamini Mkapa unaendelea kuboreshwa tayari kwa ajili ya michuano ya CHAN 2025 ambayo yatafanyika kuanzia Februari 2025 katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda

Aidha maboresho hayo ni sehemu ya maandalizi pia ya AFCON 2027 ambayo itachezwa katika ardhi ya Tanzania,Kenya na Uganda

Katika hatua nyingine, Bodi ya ligi pia imeidhinisha mchezo wa ligi kuu kati ya Singida Black Stars dhidi ya Coastal Union kupigwa katika uwanja wa New Amaan Complex, Novemba 02


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.