Liverpool wana nia ya kuboresha kikosi chao mwezi Januari na wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Ufaransa Aurelien Tchouameni, 24, kutoka Real Madrid. (Team talk)
Mshambuliaji wa Brentford na Cameroon Bryan Mbeumo, 25, na mshambuliaji wa Bournemouth wa Ghana Antoine Semenyo, 24, ni miongoni mwa wachezaji wanaowindwa na Liverpool, huku mshambuliaji wa Misri Mohamed Salah, 32, akiwa katika mwaka wa mwisho wa kandarasi yake huko Anfield. (Sky Sports)
West Ham wanataka kumsajili mshambuliaji wa Botafogo wa Brazil Igor Jesus, 23, kwa mkataba wa £30m. (Sun)
Manchester United wanataka kununua damu changa ili kumkuza na kuwa nyota katika klabu hiyo, na wanaamini kuwa mchezaji mmoja ambaye angefaa ni kiungo wa kati wa Uingereza Chris Rigg, 17, ambaye thamani ya Sunderland ni pauni milioni 20-30. (Football Insider)
Galatasaray sasa wanatumai kumsajili mchezaji anayelengwa na Chelsea Victor Osimhen kwa mkataba wa kudumu, wakiwa tayari amemchukua kwa mkopo wa msimu mzima kutoka Napoli, huku klabu hiyo ya Uturuki ikiwa tayari kulipa euro 50m (£42m) kwa mshambuliaji huyo wa Nigeria. (Sozcu)
West Ham wamejiunga na vilabu kadhaa vinavyomfuatilia winga wa Atalanta wa Nigeria Ademola Lookman, 27. (Teamtalk)
Chelsea wanatazamia kutaka kumnunua mshambuliaji wa Borussia Dortmund na Ujerumani Karim Adeyemi, 22, ambaye amekuwa akilengwa na Liverpool. (Football Insider) Matarajio ya kocha wa Bayer Leverkusen Xabi Alonso na winga wao wa miaka 21 wa Ujerumani Florian Wirtz wote kujiunga na Real Madrid yanazidi kuwa ya kweli. (Sky Sport Germany)
Real Madrid wanaweza kushindana na Arsenal na Chelsea kwa kumsajili mlinzi wa Brazil Vitor Reis mwenye umri wa miaka 18 kutoka Palmeiras. (Athletic)
Mchezaji wa Manchester City Stefan Ortega yuko kwenye rada za Bayer Leverkusen lakini bado hawajatafuta mbinu madhubuti kwa mlinda mlango huyo wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 31. (Sky Sport Ujerumani)
BBC



