Timu ya Taifa ya Tanzania imepoteza mchezo wa kuwania kufuzu CHAN 2025 dhidi ya Sudan ikifungwa kwa mikwaju ya penati 6-5 baada ya matokeo ya aggregate ya sare ya bao 1-1
Tanzania iliibuka na ushindi wa bao 1-0 katika dakika 90 za mchezo huo, Chrispine Ngushi akifunga bao la Stars katika kipindi cha kwanza akimaliza krosi ya David Bryson
Stars ilifungwa bao 1-0 katika mchezo wa mkondo wa kwanza ambao Sudan walikuwa wenyeji nchini Mauritania
Hata hivyo licha ya kupoteza mchezo huo, Tanzania inayo tiketi ya kushiriki michuano hiyo ya CHAN kama mwenyeji wa michuano hiyo ikitarajiwa kupigwa nchi za Tanzania, Kenya na Uganda mwezi February 2025
Kikosi cha Stars kinachoonyeshwa na Bakari Shime kilionyesha kandanda safi leo licha ya kujumuisha wachezaji kutoka timu ya vijana na baadhi ya wachezaji kutoka klabu za ligi kuu ukiacha wachezaji kutoka timu za Yanga, Simba na Azam Fc ambayo ilitoa mchezaji mmoja, Saadun ambaye aliingia katika dakika 20 za mwisho na kutolewa nje kwa kadi mbili za njao