Mechi mbili Ligi Kuu NBC leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th November 2024


Mechi mbili Ligi Kuu NBC leo

Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mechi mbili zinatarajiwa kupigwa mkoani Tabora na Kagera

Tabora United watakuwa wenyeji wa Maashujaa katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Ali Hassan Mwinyi saa 10 jioni

Baada ya ushindi dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo uliopita, Tabora United watakuwa wakisaka alama nyingine tatu muhimu ambazo zinaweza kuwasogeza juu ya Mashujaa katika msimamo wa ligi

Mashujaa Fc wametoka kupoteza mchezo uliopita uwanja wa nyumbani kwa kufungwa bao 1-0 na Simba, pengine hii ni mechi ya kurejea katika mwenendo wao mzuri walioanza nao msimu huu

Saa 1 usiku Kagera Sugar watakuwa nyumbani Kaitaba kumenyana na Dodoma Jiji

Kagera Sugar nayonolewa na Melis Medo wamekusanya alama tano tu katika mechi nane msimu huu, ni wazi leo watahitaji kushinda mbele timu ngumu ya Dodoma Jiji ambayo inashika nafasi ya nane katika msimamo ikiwa na alama 13


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.