International,Normal News,Liverpool

Konate atuliza presha Liverpool

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Nov 2024
Konate atuliza presha Liverpool

Ibrahima Konate amethibitisha kuwa atakuwepo kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa ya Liverpool dhidi ya Bayer Leverkusen siku ya Jumanne

Beki huyo aliwapa hofu mashabiki wa Liverpool pale alipolazimishwa kutoka wakati wa mapumziko katika ushindi wa 2-1 wa The Reds dhidi ya Brighton Jumamosi

Nafasi ya Konate ilichukuliwa na Joe Gomez baada ya kuanguka vibaya wakati wa kona, na Virgil van Dijk kisha kukanyaga mkono wake kwa bahati mbaya

"Kulikuwa na jitihada za kila mmoja kuwania mpira na nadhani nilimkanyaga kwenye mkono wake," Van Dijk alisema

"Tunatumai sio mbaya sana, itabidi tusubiri na kuona. Unaweza kuwa sawa kama mchezaji aliye na jeraha la mkono kwa hivyo tunatumai atakuwa sawa"

Mkufunzi wa Liverpool Arne Slot aliongeza: "Alikuwa na maumivu makali wakati wa mapumziko. Alikata tamaa ilibidi atoke. Bado hajalazwa hospitali. Huenda hata asiende; huwa ni mapema mno kusema baada ya mechi mchezo"

Mfaransa huyo aliondoka uwanjani akiwa ameshikilia mkono wake kwa usaidizi wa shati lake, jambo lililozua hofu kwamba huenda alivunja. Hilo lingemuacha nje ya uwanja sio tu kwa mechi ya Jumanne huko Anfield, lakini kwa muda mrefu baadaye

Kwa bahati nzuri, Konate amethibitisha kuwa amefanyiwa uchunguzi na yuko salama, atapatikana kukabiliana na Leverkusen

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
11h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
15h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
19h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
19h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
21h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
21h ago
READ MORE β†’