Kocha anayejiunga na Manchester United, Ruben Amorim, Jumanne usiku aliiongoza Sporting Lisbon katika mchezo wake wa mwisho nyumbani akiwa kocha wa timu hiyo Sporting ikiibuka na ushindi mnono kipindi cha pili na kuwashinda mabingwa wa Ligi ya Premia Manchester City 4-1 iliyosaidiwa na hat-trick ya Viktor Gyokeres
Usiku ambao presha ya kabla ya mechi iliongezeka kwa timu ya nyumbani na kocha wao mkuu aliyeondoka, City hawakuamini kilichowakumba wakiambulia kipigo cha tatu mfululizo, baada ya kupoteza Tottenham na Bournemouth
Sporting wanapanda hadi nafasi ya pili kwenye jedwali la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya nyuma ya Liverpool huku wakiendelea na mwanzo wao wa msimu bila kushindwa, huku City wakiwa nafasi ya sita baada ya kushindwa kwa mara ya kwanza katika shindano la msimu huu
Amorim, ambaye atachukua mikoba ya United baada ya wiki hii, alivumilia kipindi kigumu cha kwanza katika mchezo wake wa mwisho wa nyumbani, huku Phil Foden akitumia mwanya wa kuanza kwa wenyeji kwa kuifungia City bao la kuongoza ndani ya dakika tano baada ya kumpokonya Hidemasa Morita
Sporting wangeweza kwenda mapumziko wakiwa nyuma kwa mabao matatu lakini wakachomoa moja mwishoni mwa kipindi kupitia kwa Gyokeres, ambaye alipoteza nafasi ya kumfunga Ederson baada ya kulishwa na mlinzi wa pembeni mwenye umri wa miaka 17 Geovany Quenda
Wenyeji walirejea wakiwa bora zaidi baada y mapumziko, wakionekana kuchochewa na mazungumzo ya timu ya mapumziko kutoka kwa kocha wao mkuu aliyeondoka, walichukua uongozi sekunde 20 baada ya kuanza upya kupitia Maximiliano Araujo kabla ya Gyokeres kuongeza bao dakika nne baadaye kwa mkwaju wa penalti