Kikosi cha Tanzania 'Taifa Stars' kinahitimisha mechi za kuwania kufuzu fainali za Afcon 2025 dhidi ya Ethiopia na DR Congo
Tanzania itaanzia ugenini DR Congo kuikabili Ethiopia Novemba 16 katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Marty's Kinshasa
Ethiopia wamechagua kutumia uwanja huo katika mechi zao za mwisho dhidi ya Tanzania na DR Congo
Novemba 19 Tanzania itahitimisha kampeni yake nyumbani dimba la Mkapa kwa mchezo dhidi ya Guinea

Tanzania inapaswa kushinda mechi zote mbili ili kufuzu michuano hiyo itakayofanyika Morocco
DR Congo tayari wamefuzu kutoka kundi H wakiwa na alama 12 baada ya kushinda mechi zote nne
Guinea wako nafasi ya pili wakiwa na alama 6 wakati Tanzania iko nafasi ya tatu ikiwa na alama nne
Ethiopia wanaburuza mkia wakiwa na alama moja



