International,Normal News,Red, Barcelona

Barca yaendeleza ubabe Ulaya

Joel JJ By Joel JJ
β€’
7 Nov 2024
Barca yaendeleza ubabe Ulaya

Mshambulizi Robert Lewandowski alifunga bao katika kila kipindi na kusaidia Barcelona kupata ushindi mnono wa 5-2 dhidi ya Red Star Belgrade kwenye Ligi ya Mabingwa Jumatano

Huo ulikuwa ushindi mwingine mnono kwa vinara wa LaLiga Barcelona ambao wako katika kiwango bora, wakifunga mabao 24 katika ushindi sita mfululizo katika michuano yote, ikiwa ni pamoja na kuwazaba Bayern Munich na Real Madrid

Barca walipanda hadi nafasi ya sita kwenye jedwali la timu 36 za Ligi ya Mabingwa wakiwa na pointi tisa. Red Star wamo katika nafasi ya 35 bila pointi katika michezo minne

Meneja Hansi Flick alifanya mabadiliko mawili kwa timu ya Barcelona ambao waliwashinda wapinzani wao Espanyol 3-1 kwenye LaLiga Jumapili, na kumpa kiungo Mholanzi Frenkie De Jong mwanzo wake wa kwanza tangu apone jeraha la kifundo cha mguu

Iliwachukua Wahispania hao dakika 13 pekee kufunga bao la kwanza wakati beki Inigo Martinez alipofunga kwa kichwa mpira wa faulo uliopigwa na Raphinha dakika ya 13

Red Star wakarejea mchezoni kupitia Silas ambaye alivunja mtego wa kuotea wa Barca na kuisawazishia Red Star kwa shuti kali

Barca waliendelea kutawala mchezo na kushikilia mpango wao wakiwashinikiza wenyeji na kutengeneza nafasi kadhaa kabla ya Lewandowski kuachia shuti kali la dakika ya 43 na kuongeza uongozi wa Barca

Kipindi cha pili, Lewandowski aliongeza lake la pili likiwa la tatu kwa Barca baada ya krosi nzuri ya Jules Kounde, na dakika mbili baadaye Raphinha akaongeza la nne

Fermin Lopez aliyetokea benchi akatoa pasi nyingine kwa Kounde kuongeza bao la tano

Milson akarudisha bao moja kwa Crvena Zvezda lakini haikutosha kuzuia kipigo hicho kikubwa katika uwanja wa nyumbani

Timu hiyo ya Serbia imesalia bila pointi baada ya kipigo hicho kikali, huku Barcelona wakiwa na pointi tisa na wako mbioni kutinga raundi inayofuata

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
1m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
30m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’