Saa chache baada ya Yanga kupoteza mchezo wa pili mfululizo wa Ligi Kuu Bara kwa kipigo cha mabao 3-1 dhidi yaTabora United, Rais wa Yanga Injinia Hersi Said aliitisha kikao cha dharura na kocha wa timu hiyo, Miguel Gamondi
Kikao hicho kilimalizika usiku huku usiri juu ya kilichoamuliwa ukitawala
Baadhi ya vigogo wa klabu hiyo wanaounda Kamati ya Utendaji, Rodgers Gumbo ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano na wajumbe wengine Alex Ngai, Yanga Makaga walionekana wakitoka katika ofisi za Rais wa klabu hiyo, Injinia Hersi Said
Mbali na mabosi hao pia alikuwemo Ofisa Mtendaji Mkuu wa Yanga, Andre Mtine lakini wote hawakuwa tayari kuzungumzia lolote juu ya kilichojiri katika kikao hicho
Baada ya kuanza vyema msimu, Yanga imepoteza mechi mbili mfululizo dhidi ya Azam Fc na Tabora United zote katika uwanja wa nyumbani, Azam Complex
Jana baada ya kipigo dhidi ya Tabora United, mkufunzi wa Yanga Miguel Gamondi alisema anawajibika kwa matokeo hayo kama kocha



