Klabu za Yanga na Simba mwishoni mwa mwezi zitaanza kampeni ya hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa na kombe la Shirikisho
Yanga inayoshiriki ligi ya mabingwa itachuana na Al Hilal katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi utakaopigwa Novemba 27 katika uwanja wa Benjamin Mkapa huku Simba inayoshiriki kombe la Shirikisho, itashuka katika uwanja huo Novemba 28 kuchuana na Bravos ya Msumbiji
Bodi ya Ligi imefanya mabadiliko ya ratiba ambapo mechi za ligi zinazohusisha klabu hizo ambazo zilipaswa kuchezwa punde baada ya kukamilika mechi za kalenda ya FIFA, zimesogezwa mbele
Novemba 21 Yanga ilipaswa kucheza dhidi ya Fountain Gate na Pamba Jiji dhidi ya Simba, mechi hizo zitapangiwa tarehe nyingine
Ni wazi sasa Simba na Yanga zitakuwa na muda wa kutosha kujiandaa na mechi za CAF na pengine kuanza vyema hatua ya makundi ya michuano hiyo



