Yanga, Simba zapewa ahueni CAF

Joel JJ By Joel JJ β€’ 9th November 2024


Yanga, Simba zapewa ahueni CAF

Klabu za Yanga na Simba mwishoni mwa mwezi zitaanza kampeni ya hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa na kombe la Shirikisho

Yanga inayoshiriki ligi ya mabingwa itachuana na Al Hilal katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi utakaopigwa Novemba 27 katika uwanja wa Benjamin Mkapa huku Simba inayoshiriki kombe la Shirikisho, itashuka katika uwanja huo Novemba 28 kuchuana na Bravos ya Msumbiji

Bodi ya Ligi imefanya mabadiliko ya ratiba ambapo mechi za ligi zinazohusisha klabu hizo ambazo zilipaswa kuchezwa punde baada ya kukamilika mechi za kalenda ya FIFA, zimesogezwa mbele

Novemba 21 Yanga ilipaswa kucheza dhidi ya Fountain Gate na Pamba Jiji dhidi ya Simba, mechi hizo zitapangiwa tarehe nyingine

Ni wazi sasa Simba na Yanga zitakuwa na muda wa kutosha kujiandaa na mechi za CAF na pengine kuanza vyema hatua ya makundi ya michuano hiyo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.