Tetesi za usajili Ulaya, Jumapili Novemba 10 2024

Joel JJ By Joel JJ β€’ 10th November 2024


Tetesi za usajili Ulaya, Jumapili Novemba 10 2024

Ruben Amorim anamlenga mlinzi wa Juventus Danilo, 33, kuwa usajili wake wa kwanza Manchester United katika dirisha la Januari, kwani Mbrazili huyo anamalizia kandarasi yake mwishoni mwa msimu huu. (Mirror)

Arsenal wanamfuatilia mlinzi wa Sporting Ousmane Diomande, 20, ingawa Chelsea na Bayern Munich pia wanamtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast. (Metro)

Real Madrid wanafikiria kumsajili tena kwa dharura gwiji, Sergio Ramos, 38, huku Sevilla na beki wa zamani wa Hispania wakionekana kama mbadala wa mlinzi wa Brazil aliyejeruhiwa Eder Militao, 26. (Fichajes)

Barcelona wameondoa nia yao ya kumnunua mlinzi wa Liverpool na Uingereza Trent Alexander-Arnold, 26, ili kukidhi matakwa ya mshambuliaji wao chipukizi wa Hispania Lamine Yamal, 17. (Football365)

Meneja wa Barca Hansi Flick anataka kumsajili mlinzi Alphonso Davies, 24, ikiwa nahodha huyo wa Canada ataamua kutopokea ofa ya kandarasi kutoka kwa klabu ya sasa ya Bayern Munich - ingawa Real Madrid wanaongoza katika kinyang'anyiro cha kumsajili na Manchester United pia wanavutiwa naye. (Christian Falk, Bild)

Liverpool wako tayari kutoa ofa ya euro 70m (£58.1m) kwa ajili mshambuliaji wa Eintracht Frankfurt Omar Marmoush, 25. (Fichajes)

Mkataba wa kiungo wa kati wa Real Madrid Mfaransa Aurelien Tchouameni, 24, kujiunga na Liverpool pia unakaribia kuafikiwa. (Team talk)

Manchester City wanatumai kuimarisha safu yao ya kiungo kwa kumsajili kiungo wa kati wa Real Sociedad Martin Zubimendi, 25, ingawa Liverpool pia wanamtaka Mhispania huyo. (Football Insider)

Meneja wa zamani wa Manchester City na Italia, Roberto Mancini ndiye anayeongoza kuchukua nafasi ya Mcroatia Ivan Juric kama mkufunzi wa Roma, huku wamiliki wa klabu hiyo Marekani wakitarajiwa kuchukua hatua hiyo baada ya mechi ya Jumapili ya Serie A wakiwa nyumbani dhidi ya Bologna. (La Gazzetta dello Sport - kwa Kiitaliano)

Aston Villa wanatamani sana jozi ya Real Betis ya kiungo wa kati wa Marekani Johnny Cardoso, 23, na mlinzi wa Uhispania Diego Llorente, 31 - lakini wanatarajiwa kukabiliwa na ushindani kutoka kwa Tottenham Hotspur kuwania beki huyo. (Ficherio - kwa Kihispania)

Tottenham, West Ham na Chelsea zote zinafuatilia maendeleo ya beki wa Gent Archie Brown, 20, lakini mkataba wa Muingereza huyo katika klabu hiyo ya Ubelgiji hautaisha hadi 2027. (TBR Football)

Mshambuliaji wa Slovenia Benjamin Sesko, 21, ana "makubaliano ya kiungwana" na klabu ya sasa ya RB Leipzig kwamba ataweza kuondoka msimu wa joto ikiwa ofa itatolewa kati ya euro 70m-75m (£58m-£62m). (Philipp Hinze, Sky Sports)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.