International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu Novemba 11 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Nov 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu Novemba 11 2024

Manchester City wako tayari kulipa euro 60m (£50m) kama kipengele cha kumuachilia kiungo wa kati wa Real Sociedad Martin Zubimendi, 25, huku wakiendelea kutafuta mbadala wa Mhispania mwenzake Rodri mwezi Januari. (mirror)

Kiungo wa kati wa Real Madrid Federico Valverde, 26, ni mchezaji mwengine anayewaniwa na City lakini mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay ana kipengele cha kumuachilia cha euro 1bn (£830m). (Fichajes – In Spanish)

Paris St-Germain ni mpango B kwa fowadi wa Manchester City Erling Haaland, 24, huku Barcelona na Real Madrid pia wakimtaka raia huyo wa Norway, ambaye mkataba wake unamalizika 2027. (Soka365)

Manchester United wanataka kumnunua mshambuliaji wa Chelsea Christopher Nkunku, 26, kwani Mfaransa huyo hajafurahishwa na muda wake wa kucheza chini ya Enzo Maresca. (L'Equipe via Express)

The Red Devils pia wameungana na Barcelona katika mbio za kumnunua mlinzi wa Bayer Leverkusen wa Ujerumani Jonathan Tah, 28. (Fichajes – In Spanish)

Beki wa kati wa Tottenham na Argentina Cristian Romero, 26, na mlinzi wa Everton Mwingereza Jarrad Branthwaite, 22, wametambuliwa na Real Madrid kama wachezaji wanaoweza kuwaimarisha. (Caught Offside)

Kiungo wa kati wa Liverpool Wataru Endo, 31, anahitajika sana huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Japan akiendelea kutatizika kwa muda wa mechi huko Anfield, huku AC Milan, Fulham, Wolves na Ipswich zikiwa na nia ya kumnunua. (Caught Offside)

Tottenham wanatamani kumnunua kiungo wa kati wa Argentina Facundo Buonanotte, 19, lakini watalazimika kushindana na Leicester. Kwa sasa mchezaji huyo yuko kwa mkopo. (Fichajes – In Spanish)

Mkurugenzi wa Santos Marcio Calves anasema kurejea kwa Neymar, 32, katika klabu yake ya zamani itakuwa "ndoto ya kila shabiki" na ingawa hakuna "mazungumzo rasmi" yaliyofanyika na klabu ya sasa ya Al-Hilal, alikuwa na uhakika "60%" kwamba mshambuliaji huyo wa Brazil atakamilisha uhamisho mkataba wake utakapokamilika mwezi Juni (Mundo Deportivo – In Spanish)

Roberto Mancini ndiye anayepewa nafasi kubwa ya kuteuliwa kuwa meneja wa Roma lakini mabosi wa zamani Daniele de Rossi na Claudio Ranieri wanasalia kwenye mfumo huo, huku Frank Lampard pia akihusishwa na nafasi hiyo iliyo wazi. (La Gazzatta Dello Sport – In Italy)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’