Nyota wa Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' Saimon Msuva ameripoti kambini akiungana na wachezaji wenzake kwa ajili ya maandalizi ya michezo miwili ya kufuzu AFCON 2025, dhidi ya Ethiopia na Guinea itakayochezwa Novemba 16 na Novemba 19, 2024
Baada ya kukosekana katika mechi nne zilizopita, hatimaye Msuva ambaye sasa anacheza soka la kulipwa huko Iraq, amerejea kuendeleza kasi yake ya kutupia mabao muhimu katika kikosi cha Stars
Tanzania itahitaji maajabu yake katika mechi hizo mbili ambazo Stars inahitaji kushinda ili iweze kufuzu Afcon 2025