Bodi ya Ligi imefanya mabadiliko kwenye mchezo namba 89 kati ya Pamba Jiji FC dhidi ya Simba SC, uliokuwa haujapangiwa tarehe baada ya kuondolewa Novemba 21, 2024
Mchezo huo sasa utachezwa Novemba 22, 2024 saa 10:00 jioni katika Uwanja wa CCM Kirumba
Simba ilipeleka maombi TPLB ikiomba mchezo huo upigwe kama ratiba ilivyokuwa imepangwa awali
Pamba Jiji wamethibitisha kupokea taarifa ya mabadiliko hayo kutoka kwa Bodi ya Ligi




